body{background: #ededed;margin:0;padding:0;}#menu_wrap{position:relative;margin-top:20px;margin-le

HISTORIA

KOFFI ANNAN
        Alizaliwa Aprili 8,1938 huko Kumasi nchini GHANA .Alizaliwa katika familia maarufu na baba yake alikuwa ni Chifu wa kabila la Fante na akiwa kama mtumishi mkubwa katika serikali. Annan alibahatika kupata nafasi ya kusoma akijushughulisha na masuala ya sayansi na teknolojia nchini Ghana.Mwaka 1959 alipata nafasi ya kwenda kusoma Nchini Marekani katika chuo cha Macalaster huko S.Paul Minnesota. Mwaka 1961 alipata shahada yake ya kwanza katika masuala ya uchumi huko Macalaster. Baadaye alienda kusoma Geneva,Uswisi na kupata shahada nyingine ya Masuala ya uchumi .
     Alipata kazi yake ya Kwanza jumuiya Ya Madola katika Shirika la Chakula Duniani (WHO), Aliacha kazi UN na kufanya kazi katika kampuni ya maendeleo ya utalii nchini Ghana ambapo alifanya kazi hapo kuanzia 1974 hadi 1976. Miaka minne baadae . baadaye aliteuliwa tena na UN kama Naibu Kiongozi mkuu wa shirika la wakimbizi ambapo alifanya kazi mpaka ilivyofika mwaka 1983 alipoteuliwa kuwa mkuu wa idara ya fedha. Mwaka 1990 kofi annan  alipandishwa cheo na kuwa assistant katika upangaji w bajeti na matumizi ya UN.ilivyofika mwaka 1993 liteuliwa kuwa kionhozi mkuu wa mazungumzo ya amani wa Umoja wa Mataifa.

        Kofi annan ni mwafrika wa kwanza kuwa katibu mkuu wa kwanza wa jumuiya ya madola (UN) akiichukua nafasi hiyo Januari 1997 mpaka Disemba 31,mwaka 2001. Annan alisifika sana kimataif na katika jumuiya ya madola akwa uwezo wake mkubwa wa usuluhishi  wa migogoro ya amani akiwa kama Katibu Mkuu wa jumuiya ya madola. Umashuhuri wake na uwezo aliokuwa nao ulimsaida katika nchi kama Rwanda,Somalia na hoko Yugoslavia.

No comments:

Post a Comment